Social Icons

Tuesday 18 October 2016

Vyuo vikuu vyote nchini kuhakikiwa

Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255629914471. insta : @matukionawanavyuo Tumieni mtandao huu ni wenu nyote. 

WIZARA ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi inatarajia kuvifanyia uhakiki wa ubora ubora vyuo vyote, vinavyotoa shahada nchini vya umma na vya binafsi kuanzia kesho.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Maimuna Tarishi, vyuo vyote vinatakiwa kutoa ushirikiano kwa timu za wataalamu, zitakazofika kwa ajili ya kufanya uhakiki huo.
Aidha, Tarishi alisema katika ukaguzi wa sifa za wanafunzi wanaoendelea na masomo, vyuo vyote pamoja na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), leo vitatoa majina ya wanafunzi wanaotambuliwa na kwamba walidahiliwa kupitia TCU.
“Hivyo, wanafunzi wote wanatakiwa kuangalia majina yao katika Tovuti ya TCU na kwa yeyote ambaye hataona jina lake awasiliane na uongozi wa TCU haraka iwezekanavyo ili kupata maelezo zaidi,” alisema Katibu Mkuu huyo.
Alisisitiza kuwa mwanafunzi yeyote ambaye hatazingatia maagizo hayo ndani ya wiki mbili atapoteza sifa za kuendelea na masomo.
Hivi karibuni, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, alitangaza kuanzisha msako wa wanafunzi hewa vyuoni baada ya kubainika kuwepo kwa wanafunzi hewa wanaopewa mikopo wakiwemo wengine wanaosoma shahada huku wakiwa hawana sifa.
CHANZO GAZETI LA HABARI LEO

No comments: