Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
Na Eleuteri
Mangi-MAELEZO
Wanafunzi wenye
mahitaji maalum wanaosoma vyuo vikuu nchini wameaswa kutumia elimu wanayoipata kuendesha
maisha yao ili waweze kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla.
Hayo yamesemwa na Prof.
Mshiriki wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Kituo cha Studi za Mawasiliano Martha
Qorro ambaye alikuwa Mgeni Mashuhuri wakati wa Mahafali ya nane ya Chuo Kikuu
Kishiriki cha Elimu Dar es Salaama (DUCE) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki
jijini Dar es salaaam.
Prof. Qorro alisema kuwa
mwamko wa wanafunzi wenye mahitaji maalum kujiunga na elimu ya juu nchini ni mzuri
licha ya changamoto zinazowakumba wanafunzi hao wanapokuwa chuoni.
“Hawa ni wanafunzi
wenye uelewa mzuri wakipata mahitaji yao ya lazima yakiwemo fimbo nyeupe, vifaa
vya kuandikia kwa kutumia nukta nundu, baiskeli za miguu mitatu, viti maalu na
mahitaji mengine ya kijamii” alisema Prof.Qorro.
Prof.Qorro aliongeza
kuwa ni wajibu wa vyuo vikuu nchini kikiwepo Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar
es Salaam kuwasisitiza kwa kuwauliza wanafunzi wanapojaza fomu za kujiunga
waoneshe kuwa wanamahitaji maalum ili waandaliwe mahitaji hayo ikiwemo usafiri
wa bajaji ndani ya chuo ili kuwawezesha kuwahi vipindi vyao katika maeneo
mbalimbali ndani ya chuo.
Kwa upande wake Mkuu wa
Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Profesa William Anganisye alipokuwa
akitoa taarifa fupi kuhusu mafanikio chuo wakati wa Mahafali hayo alisema kuwa chuo
hicho kimetimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake ambapo hadi sasa wamehitimu
wanafunzi zaidi ya 8000 na jumla ya wahitimu 1156 walitunukiwa Shahada na
Stashahada za juu katika mahafali hiyo ya nane.
Naye muhitim wa mwaka
wa tatu katika ngazi ya shahada ya ualimu katika masomo ya sanaa Andrea Sanga ambaye
pia ni mwanafunzi mwenye mahitaji maalum (mlemavu asiyeona) alisema kuwa mafanikio
yake katika masomo yametokana na kuheshimu ratiba kuu ya masomo chuoni hapo pamoja
na ratiba yake binafsi ya kujisomea.
Zaidi ya hayo, Sanga
alisema kuwa maktaba ya chuo, ushirikiano mzuri kati yake na wanafunzi wenzake
na walimu wake, kuhudhuria semina na kufanya kazi kwa wakati na kupunguza
msongamano wa kazi nyingine ndiyo vimekuwa dira yake kuu ya mafanikio.
No comments:
Post a Comment