Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
Kamati hiyo ina wajumbe 32 wanaoongozwa na Katibu Mkuu.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana,
alisema timu ya CCM imeundwa na makada wenye uwezo mbalimbali wakiwamo
wa kurusha makombora makali kwa upinzani.
Alisema: “Unaweza kuona kamati hii ilivyopangwa imekamilika kwa
sababu kuna watu wa kutoa mapigo na wenye busara kama akina Kinana
(Abdulrahman) wa kuweka mambo sawa.” Alisema kamati ya CCM imezingatia
hali ya kisiasa nchini na nguvu kubwa ya upinzani iliyopo akiwataja
baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo wenye uwezo wa kurusha makombora kwa
upinzani kuwa ni Nape Nnauye, Dk. Harrison Mwakyembe, Samuel Sitta na
Livingstone Lusinde.
Mhadhiri mwingine wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Haji
Semboja, alisema kamati hiyo itaweza kufanyakazi yake kwa urahisi kama
mategemeo ya wananchi katika kipindi cha miaka 10 ya utawala wa Rais
Jakaya Kikwete, ulizingatia maslahi ya umma.
Alisema pia kuwa timu hiyo ina jukumu kubwa la kuushawishi umma
umchague mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli, kwa kuwa anakabiliwa
na upinzani mkali kutoka kwa Edward Lowassa, anayepeperusha bendera ya
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
“Wananchi wanataka mabadiliko na wanaamini kuwa Magufuli na Lowassa
ni watendaji wazuri kwa hiyo wananchi wanahitaji kujua ni kwa namna
gani rais ajaye atatekeleza changamoto zinazowakabili …siyo suala la
sera wala sheria kwa sababu tayari zipo nzuri,” alisema.
Dk. Semboja alisema kampeni za mwaka huu zinahitaji wagombea na
timu zao kuzungumzia matakwa ya wananchi badala ya matusi au kejeli.
Bashiru Ali kutoka UDSM, alisema uteuzi wa mwaka huu uliohusisha
watu wa makundi mbalimbali utasaidia kuvunja makundi ndani ya chama
tawala.
“Na hii itatimiza kauli ya CCM ya umoja ni ushindi,” alisema.
Naye Mhadhiri mstaafu wa UDSM, Prof. Gaudence Mpangala, alisema
uwingi wa makada wanaounda timu ya kampeni ya CCM siyo kigezo cha
kuibuka na ushindi, bali wazungumzie sera za chama chao na siyo kutoa
kauli za kuchafuana.
Kamati hiyo ina wajumbe 32 wanaoongozwa na Katibu Mkuu, Kinana.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment