Kufuatia kufanya vizuri kwa Shule ya Sekondari ya St. Joseph
ya Jijini Dar es Salaam ambayo inamilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo Kuu
la Dar es Salaam, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es
Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo Julai 18, mwaka huu alikutana
na wanafunzi wa tatu walioongoza Kitaifa na kuongoza kwa masomo na
kuwapa pongezi.
Pichani juu ni Muadhama Polycarp Kardinali Pengo, akisalimiana
na wanafunzi waliofanya vizuri kitaifa kutoka shule ya Sekondari ya
St. Joseph Cathedral ya Dar es Salaam ambayo inamilikiwa na Kanisa
Katoliki ambao ni , Joseph Ngobya wa masomo ya Sanaa na Lugha, Isaack
Shayo aliyeshika namba moja kitaifa (katikati) na Prince Mwambaja
(wapili kushoto) aliyeshika nafasi ya tano kitaifa masomo ya biashara.
Mwalimu Mkuu,Sr. Theodora Faustine akizungumza wakati wa mkutano huo.
Wazazi walimpa Kardinali zawadi kwa kuanzisha shule hiyo na kutoa elimu kwa vijana wao.
Sr. Theodora Faustine ambaye ndio Mkuu wa shule ya Sekondari ya St. Joseph Cathedral akizungumza.
Wanafunzi wakiwa katika Mkutano huo wa shukrani kwa Kardinali Pengo.
Picha ya pamoja kati ya wahitimu na Kardinali Pengo na familia ilipigwa.
Wahitimu wakizungumza yao.
Wahitimu wakiwa na mwalimu wao Mkuu, Sr. Theodora Faustine.
Kwa hisani ya Father Kidevu Blog
Kwa wanavyuo wote watanzania popote Duniani Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Tumieni mtandao huu ni wenu nyote.
No comments:
Post a Comment